Ibada tarehe : 21/8/2021 Somo : UHARIBIFU

 

MCHUNGAJI,

 VICTOR GASPER MALAMLA.
 
1Wakorintho 10:10, "Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu."
Yohana 10:10, "Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele."
 
Nini maana ya uharibifu?Uharibifu ni roho inayoondoa ukamilifu wa Mungu. Mungu ametuumba wakamilifu, amefanya kila kitu kwa ukamilifu. Anayeharibu na kutoa ukamilifu ni adui (shetani) ili tushindwe kufanya yaliyo mapenzi ya Mungu.
 
Maana ya pili ya uharibifu ni; roho inayovuruga utaratibu na mpangilio wa Mungu kwenye maisha ya kila siku ya wanadamu. Kazi ya roho ya uharibifu ni kuvuruga mpangilio uliopo, kila mtu anakuwa anafanya anachokitaka yeye. Hata kama ni kanisani kunakuwa na uvunjifu wa mipangilio na miongozo yote iliyopo mahali hapo. 

Maana ya tatu ya uharibifu ni; roho yenye nguvu ya mauti na kuua, inaua mwili, kazi, elimu, biashara, ndoa na afya. Popote palipo na roho ya uharibifu kunakuwa na mauti. Ukiona kila unachofanya hakisongi mbele basi ujue kuna uchawi ndani yake

Anaeharibu anaitwa mharabu. Shetani anatenda kazi katika roho ya uharibifu, ili uharibifu wa shetani utokee kwenye kazi, biashara, taifa, elimu na mahali popote  kitendea kazi chake ni uchawi. Uharibifu na uchawi ni vitu vinavyoenda sambamba. Mtu anayefanya kazi na shetani anaweza kufanya uharibifu mahali popote. Mtu mchawi anaweza akaenda kanisani na kunena kwa lugha kama wengine, lakini kwa mganga ni ngumu sana. Kuna mahali hawezi kwenda na akienda mahali hapo basi kazi zake zote zinaharibika. 

Muhimu kufahamu ni;
 
-Uganga ni kiwango cha chini cha uchawi, waganga wote wanaripoti kwa wachawi.
-Matambiko ni uchawi.
- Mila na desturi ni uchawi. Uchawi umebeba vipengele vingi sana ndani yake.

Ukiona mtu anatamani kuacha uzinzi, kiburi, hasira, uasherati, ulevi na masimango na hawezi basi ujue kuna uchawi ndani yake. Kiburi ni chanzo cha mafarakano na migogoro katika ndoa nyingi. Uchungu ni roho ambayo inatumwa kwa mtu ili ashindwe kusamehe, na mtu akishindwa kusamehe basi hawezi kusamehewa na hapo anakuwa amefungua mlango kwa ajili ya adui kupandikiza mateso kwake. 

Kushinda vita vya kichawi ni lazima ushughulike na moyo kwanza. Na jambo hili sio la siku moja anayeweza kukusaidia ni Roho Mtakatifu, mwambie akufundishe kusamehe na uondokane na hali ya kutokusamehe (gubu). Sio kila tabia ambayo mtu anayo ni ya kwake zingine zinatokana na uchawi.
 
 
ILI UWEZE KUSHINDA UCHAWI NI LAZIMA;

1. Uepukane na uchungu, jifunze kuwa mtu wa kusamehe na kuachilia watu kwa kadri unavyowashikilia watu ndivyo unavyozidi kufungua mlango kwa ajili ya mateso, magonjwa na maumivu mengi kwako. Ni lazima uweze kuutiisha mwili wako ili uweze kukutana na Roho wa Mungu.

2Wakorintho 5:17, "Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya."

Kiumbe kipya ni roho yako, kazi ya uchawi ni kupambana na roho yako ili isiweze kushabihiana (kuendana) na mwili wako. 

Ili yale unayoyaona katika roho yadhihirishwe katika damu na nyama ni lazima ushinde uchawi. Bila mtu kuushinda uchawi hawezi kufikia makusudi ya Mungu. 

2. Kufunga na kuomba ni lazima ili uweze kuushinda uchawi. Hauwezi kukwepa kufunga na kuomba kama unatamani kufikia makusudi ambayo Mungu ameweka kwako.

Mtu asipofanya maamuzi ya kuutisha mwili wake kuushinda uchawi ni ngumu mno. Hauwezi kwenda mbinguni ukaketi kama haujashinda hapa duniani. Kila mwamini lazima aoneshe ushindi wake kupitia Yesu.

Mika 5:12-15, "nami nitakatilia mbali uchawi, usiwe mkononi mwako; wala hutakuwa tena na watu wenye kutabana..."

Kuna mambo manne MUNGU anashughulika nayo;

1. Anashughulika na roho zote za uchawi.
2. Anashughulika na sanamu na nguzo, vitu ambavyo vinatunza uchawi.
3. Anavunja madhabahu na kukomesha kazi zao.
4.  Anashughulika na watu wanaotenda au kumiliki huo uchawi.

KANISA LA EFATHA NUNDU MWANZA
 
 
 
 
 
 
 
 

Comments

Popular posts from this blog

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 28.08.2022, SOMO : ROHO YA UCHAWI

Ibada Tarehe 14/8/2022, SOMO : UONGOZI