IBADA YA JUMAPILI TAREHE 28.08.2022, SOMO : ROHO YA UCHAWI
MCHUNGAJI VICTOR GASPER MALAMLA Wagalatia 3:1-3, "Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa?.." Ili mwamini aweze kushinda roho ya uchawi ndani yake ni lazima 1. Ajifunze kutii kwa ukamilifu ndani yake. Wachawi wanapata nafasi kwa watakatifu kutokana na kushindwa kuwa watii. Kutokana na kiwango cha utii ulichonacho unaweza kufukuza mapepo kila mahali. Muda mwingine hauitaji kuomba ila kwa utii wako tu unaweza kushinda. Kwa kadri unavyoelekezwa na kutii, unaweza kutiisha kila kitu yani viumbe hai na visivyo hai. Usipokuwa mtii kwenye mapato, hauwezi kupata mafanikio. Ili Mungu akupe baraka zinazokutofautisha na wengine ni lazima uwe mtii katika mapato. Hapo ulipofikia leo ni kwa sababu neema ya Mungu ni kubwa na imekufikisha hapo. Isaya 1:19, "Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi;" Ukiona umeokoka halafu ghafla una...